Mwananchi Communications LTD BLOG
Mafunzo ya wanafunzi kwa vitendo
- Details
- Created on Friday, 24 May 2013 08:38
- Hits: 2

Wanafunzi wa shule ya msingi Haydom Wilayani Mbulu Mkoani Manyara wakijifunza kutengeneza nishati ya mkaa mbadala kwenye Kituo cha pembe nne za utamaduni Haydom (4CCP) juzi kwa lengo la kutunza mazingira.Picha na Joseph Lyimo
''Tutafika mdogo mdogo''
- Details
- Created on Friday, 24 May 2013 08:36
- Hits: 4

Daladala likipita katika njia inayoungnisha Kimara na Bonyokwa nje kidog ya jiji la Dar es Salaam jana, barabara hiyo iliyojengwa kwa kiwango cha changarawe na mifereji mwezi wa tatu kwa sasa inapitika kwa shida baada ya sehemu nyingi kuharibika kutoka na ujenzi kutozingatia utaalumu wa kutosha. Picha na Salhim Shao
''Hatutaki watalii!''
- Details
- Created on Friday, 24 May 2013 08:34
- Hits: 8

Wananchi wanaoishi ndani ya eneo la Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro katika kijiji cha Olbalbal wakiwa kwenye kikao walichokubaliana kuzuia watalii kuingia katika hifadhi hiyo kwa kufunga geti iwapo serikali haitatekeleza matakwa yao. Picha na Mussa juma
''hali sio nzuri''
- Details
- Created on Friday, 24 May 2013 08:31
- Hits: 3

Mvuvi wa samaki kwenye Ziwa Bassotu, mkoa wa Manyara,Charles Manyama akizungumzia hali kipato chao kuyumba baada ya Ziwa hilo kufungwa kwa muda ili kuwezesha samaki kuongezeka.Picha na Filbert Rweyemamu
Bungeni laendelea
- Details
- Created on Thursday, 16 May 2013 08:46
- Hits: 76

Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Kessy akiwa amefumba mdomo wakati bunge lilipokuwa limekaa kama kamati kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2013/14, mjini Dodoma jana. Kushoto ni Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe akifurahi wakati Kessy alipokuwa akifanya tukio hilo. Picha na Edwin Mjwahuzi
"Hongera Waziri"
- Details
- Created on Thursday, 16 May 2013 08:45
- Hits: 40

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (mwenye tai nyekundu) akipongezwa na wabunge pamoja na mawaziri baada ya kupitishwa kwa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/14, mjini Dodoma juzi. Picha na Edwin Mjwahuzi
"Pumzikeni kwa amani"
- Details
- Created on Thursday, 16 May 2013 08:44
- Hits: 32

Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada,John Baird(kushoto)akiweka shada la maua jana kwenye makaburi ya watu watatu waliouawa kwenye tukio la shambulio la bomu kwenye kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti,jijini Arusha Mei 5,mwaka huu.Picha na Filbert Rweyemamu
Faida za virutubisho katika vyakula
- Details
- Created on Thursday, 16 May 2013 08:41
- Hits: 31

Ofisa wa Lishe kutoka katika Sekta ya Maendeleo na Menejimenti za Afya, Leticia Chang’a akiwaelezea faida za virutubisho katika vyakula wakazi wa jiji la Dar es Salaaam walitembelea maonesho ya lishe jana yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja. Picha na Venance Nestory
"Tunalinda mazao"
- Details
- Created on Thursday, 16 May 2013 08:39
- Hits: 29

Wakulima wa mpunga katika kijiji cha Mgungila mkoani Singida wakiwa kwenye lindo la kuwafukuza ndege ambao wamekuwa wakila mpunga huo, ambapo wamesema bila ya kulinda wanaweza kumaliza shamba lote.Picha na Masoud Masasi
Mkagangamale vijana
- Details
- Created on Thursday, 09 May 2013 08:53
- Hits: 77

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi bendera kiongozi wa batalioni ya wanajeshi wa JWTZ wanaokwenda kujiunga na jeshi la Umoja wa Mataifa la kulinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, katika sherehe za kuwaaga zilizofanyika Msangani, Kibaha, Mkoa wa Pwani jana. Picha na Ikulu
Msaada wa blanketi
- Details
- Created on Thursday, 09 May 2013 08:51
- Hits: 36

Mbunge wa Kishapu mkoani Shinyanga Suleiman Nchambi akikabidhi blanketi kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea katika Vijiji vitatu vya Mwanhili Mwasubi na Itongoitale katika kata ya Bunambiyu Tarafa ya Mondo wilayani Kishapu.
Uzinduzi wa ilani ya madai kwa wanawake
- Details
- Created on Thursday, 09 May 2013 08:49
- Hits: 35

Wananchi wakiwa katika maandamano jana kabla ya uzinduzi wa ilani ya madai ya wanawake wa Tanzania katika katiba mpya iliyotayarishwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) jijini Dar es salaam. Picha na Aika Kimaro
Ulinzi mkutanoni
- Details
- Created on Thursday, 09 May 2013 08:48
- Hits: 44

Wakazi wa manispaa ya Singida mkoani humo wakimsikiliza katibu mkuu wa chama cha CUF,Seif Sharrif Hamad katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi.Picha na Gasper Andrew.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknollojia
- Details
- Created on Wednesday, 08 May 2013 14:08
- Hits: 36

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknollojia, Prof. Makame Mbarawa akiongea na mmoja wa wajasiliamali kwenye semina iliyoandaliwa na Dar Teknohama Business Incubator (DTBi) chini yaTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na taasisi ya GIST ya Marekani kwa ajili ya kuwapa mbinu mbalimbali za kijasiliamali. Picha na Rafael Lubava
Balozi wa Marekani
- Details
- Created on Wednesday, 08 May 2013 14:03
- Hits: 36

Balozi wa Marekani nchini, Alfonso E. Lenhardt akizungumza kwenye semina ya wajasiliamali
Mkurugenzi Mkuu waTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)
- Details
- Created on Wednesday, 08 May 2013 14:00
- Hits: 37

Mkurugenzi Mkuu waTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dr. Hassan Mshinda akizungumza kwenye semina ya siku mbili kwa ajili ya wajasiliamali iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Semina ya ujasiliamali
- Details
- Created on Wednesday, 08 May 2013 13:57
- Hits: 42

wajasiliamali mbalimbali wakifuatilia semina Iliyoandaliwa na Dar Teknohama Business Incubator (DTBi) chini yaTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na taasisi ya GIST ya Marekani. Picha na Rafael Lubava
Tunakoelekea.........!
- Details
- Created on Monday, 06 May 2013 08:32
- Hits: 52

Majeruhi wakiwa kwenye hospitali ya mkoa wa Mount Meru wakipata matibabu kutokana na kushambuliwa na mtu asiyejulikana na kitu kinachosadikiwa ni Bomu la kurushwa kwa mkono wakati waumini hao walipokuwa kwenye ibada ya uzinduzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakifu Joseph Mfanyakazi,Jimbo Kuu la Arusha jana. Mtu mmoja amefariki na 61 kujeruhiwa. Picha na Filbert Rweyemamu

Viatu vya watu waliopata madhara ya mlipuko wa bomu

Maafisa wa Polisi wakichunguza milipuko kwenye eneo la Kanisa

Mtoto aliyejeruhiwa akipata matibabu

Jengo la Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi,Jimbo Kuu la Arusha lililokuwa lizinduliwe jana na Balozi wa Vatican na Mjumbe Maalumu wa Papa,Askofu Mkuu,Fransis Padilla. Shughuli hiyo ilisitishwa baada ya mtu asiyejulikana kurusha kitu kinachosadikiwa ni Bomu na kuua mtu mmoja na kujeruhi 61.
Maadhimisho ya Albino
- Details
- Created on Monday, 06 May 2013 08:22
- Hits: 33

Wananchi wakishiriki kwenye maandamano ya kilele cha maadhimisho ya siku ya walemavu wa ngozi (albino) yaliyofanyika mkoani Singida juzi. Picha na Gasper Andrew
Kufa kupona
- Details
- Created on Monday, 29 April 2013 08:46
- Hits: 59

Mshambuliaji wa Atletico Madrid raia wa Kolombia, Radamel Falcao (katikati) akigombania mpira na winga wa Real Madrid, Kaka (kushoto) na beki, Ricaldo Calvalho kwenye mechi ya ligi kuu ya Hispania katika uwanja wa Vicente Calderon, Madrid juzi, Real Madrid ilishinda 2-1. Picha na AFP
Madhara ya vurugu
- Details
- Created on Monday, 29 April 2013 08:33
- Hits: 52
Wakazi wa Liwale, wakiondoa mabaki ya dawa za kilimo mali ya Makamu Mwenyekiti wa chama cha msingi cha Umoja,Hasani Mpako, zilizoteketezwa kwenye nyumba yake, wakati wa vurugu zilizotokea wiki iliyopita, watu 31 wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo, kujibu tuhuma kuhusiana na vurugu hizo. Picha na Christopher Lilai
Kibaka
- Details
- Created on Monday, 29 April 2013 08:30
- Hits: 57

Wanausalama wakimdhibiti kijana anayedaiwa kuwa ni kibaka, baada ya kumkwapulia simu abiria aliyekuwa ndani ya daladala wakati likitembea, mjini Morogoro jana. Uporaji umekuwa ukiongezeka siku hadi siku hasa katika maeneo ya mijini. Picha na Juma Mtanda
Taka barabarani
- Details
- Created on Monday, 29 April 2013 08:28
- Hits: 43

Taka zikiwa zimelundikwa katika barabara inayojengwa ya mradi wa Mabasi yaendayo Kasi (DART), eneo la Magomeni Kagera Dar es Salaam jana. Mradi huo umekuwa ukikumbana na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na machinga kuvamia eneo la mradi na uhalibifu wa miundombinu unaofanywa na madereva wanaokwepa foleni. Picha na Venance Nestory
Msaada wa madawati
- Details
- Created on Monday, 29 April 2013 08:25
- Hits: 40

Mwananfunzi wa darasa la tau wa shule ya msingi Misuna ya Singida, Athumani Jingu na Mkuu wa mkoa wa Sindida, Dk.Parseko Kone (kushoto) wakipoea sehemu ya madawati 264, kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemia Mchechu wa pili (katikati), na makamu mwenyekiti wa Hassan Maajar Trust (HMT), Shariff Maajar (wa pili kulia), kwenye hafla iliyofanyika mjini Singida, Madawati yaliyotolewa na NHC. Kulia ni Ofisa balozi Bertha Sami. Picha na Gasper Andrew.
Buriani Bi Kidude
- Details
- Created on Thursday, 18 April 2013 08:54
- Hits: 1073

Msanii mkongwe wa nyimbo mbalimbali zikiwemo za asili, Fatma binti Baraka 'Bi Kidude' amefariki jana mara baada ya kusumbuliwa na maradh mbalimbali kwa muda mrefu.
Heshima za mwisho
- Details
- Created on Tuesday, 16 April 2013 08:50
- Hits: 112

Viongozi na wananchi wakiwa wamesimama mbele ya jeneza lililokuwa na mwili wa Mkuu wa zamani wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Makame Rashid, Makao makuu ya Jeshi hilo Mlalakuwa Dar es Salaam, kabla ya za mwisho jana. Picha na Rafael Lubava
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (JWTZ) Davis Mwamunyange akitoa heshima za mwisho
- Details
- Created on Tuesday, 16 April 2013 08:44
- Hits: 613

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (JWTZ) Davis Mwamunyange akitoa heshima za mwisho kwenye jeneza lililokuwa na mwili wa Mkuu wa zamani wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) Meja Jenerali Makame Rashid, Makao makuu ya Jeshi hilo Mlalakuwa Dar es Salaam, jana. Picha na Rafael Lubava
Adha ya upanuzi wa barabara
- Details
- Created on Tuesday, 16 April 2013 08:36
- Hits: 70

Wakazi wa Mianzini, mkoani Arusha wakipita kandokando ya nyumba zilizokuwa zikivunjwa ili kupanua barabara ya Mianzini hadi Sambasha yenye urefu wa kilomita 19. 7. Picha na Moses Mashalla
Lori lamlazimisha mwananchi kukaa banda
- Details
- Created on Tuesday, 16 April 2013 08:30
- Hits: 83

Lori likiwa limeparamia migomba na kupinduka wilayani Ngara, Mkoani Kagera na kujeruhi watu kadhaa na kuharibu nyumba ya Bibiana John ambaye amelazimika kukaa katika banda la muda. Picha na
Ajali ya ndege yamuua Bob Sambeke
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:40
- Hits: 223

Wananchi wakiangalia ndege aina ya Cessna 5H-QTT ikiwa imeanguka eneo la Kisongo, karibu na Uwanja wa ndege wa Arusha juzi, baada ya kugonga mti wakati ikijiandaa kutua na kusababisha kifo cha mmiliki wake na aliyekuwa rubani, Bob Sambeke. Picha na Filbert Rweyemamu
Msaada kwa wananchi
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:35
- Hits: 68

Wananchi wa vijini vya Itongo itale na Mwanhili Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga, waliokumbwa na maguriko na kupoteza nyumba, vyakula na mifugo, wakimsikiliza mkuu wa mkoa Ally Rufunga alipowatembelea na kutoa ahadi ya sh16.6 za kuwasaidia. Picha na Suzzy Butondo
Chanjo ya mbwa
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:31
- Hits: 61

Afisa Mifugo wa Kata ya Ukonga Fatuma Hassan, akitoa chanjo ya kichaa cha mbwa katika Kata ya Msongola, Ilala Dar es Salaam juzi, ili kudhibiti ugomjwa huo unaombukizwa kutoka kwa mbwa kwenda kwa binadamu, endapo atang’atwa na mnyama mwenye ugonjwa. Picha na Pamela Chilongola
Sala ya mazishi
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:29
- Hits: 69

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Muhidin Ndolanga (kushoto) akishiriki kisomo cha kumwombea Marehemu Meja Jenerali Makame Rashid ambaye aliwahi Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Balozi wa Tanzania nchini Malawi aliyefariki jana Dar es Salaam. Anatarajiwa kusafirishwa kwenda kuzikwa wilayani Tandahimba baada ya taratibu zote za kuaga kukamilika.Picha na Salhim Shao
Gesi asilia
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:27
- Hits: 65

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, akiwakilisha mada kuhusu gesi asilia wakati wa kongamano la Chama hicho, mjini Mtwara juzi. Picha na Abdallah Bakari
Gari juu ya mkokoteni
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:26
- Hits: 68

Wakazi wa mjini Singida, wakijaribu kuongoza mkokoteni unaonekana kuwashinda nguvu wakati wakihamisha bodi ya gari kama walivyokutwa jana. Picha na Gasper Andrew
Rais na raia wake
- Details
- Created on Monday, 15 April 2013 08:24
- Hits: 53

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Kasera Wilayani Mkinga, Mkoani Tanga, baada ya kuzindua mpya ya rami yenye urefu wa km 60 kutoka Tanga hadi Horohoro, mpakani mwa Kenya, iliyojengwa ufadhili wa mfuko Marakeni wa Millennium Challenge Corporation (MCC). Picha na Salim Mohammed
BAKWATA YAUNGA MKONO UCHINJAJI
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:33
- Hits: 223

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salim akiongea na waandishi wa habari jijini hapa jana kuhusiana na mambo mbalimbali yaliyojitokeza na kuhatarisha amani na kusema ili kuyaepusha ni vizuri viongozi wa dini kukutana mara kwa mara. Picha na Rafael Lubava
BAKWATA YAMUUNGA MKONO MWINYI
Rafael Lubava. Mcl blog
Balaza Kuu la Waislam nchini (BAKWATA) limeunga mkono kauli ya Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi kuhusiana na uhuru wa kuchinja na kusema ni vizuri kufuata utaratibu uliokuwepo kwani hauna kasoro ili kudumisha amani.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa huu, Alhad Mussa Salim alisema ni vizuri kufuata utaratibu wa mtu kujichinjia kinachotumika na familia lakini kama cha jamii kwa ujumla ufuatwe ule wa zamani.
‘’Mkristo ajichinjie anachotaka ale vile vile na Muislamu naye afanye hivyo kwa kile kinacholiwa kifamilia, lakini kama ni kwa ajili jamii nzima, jamani tuendelee tu kufuata tu utaratibu uliopo’’ Alisema na kuongeza.
‘’Mkristo hana mwiko kula kilichochinjwa na Muislamu na ndivyo ilivyokuwa miaka yote ambapo nyama inayotakiwa itumike na jamii imekuwa ikichinjwa na Waislamu na tumeishi hivi bila shida yoyote kwa miaka yote’’
Pamoja na hayo Sheikh Salim alisema tatizo kubwa linalosababishwa uwepo wa migogoro nchini ni kutokutana mara kwa mara kwa viongozi wa dini ili kujadili na kutatua tofauti zao kabla hazijaeta madhara.
‘’Viongozi hawakutani mpaka migogoro itokee, hivyo hata kama kuna vuguvugu za chini kwa chini ni vigumu kujua, unakuja kugundua tayari hali ni mbaya na inakuwa ni vigumu sana kurejesha amani mapema’’.
Alimsifu pia Rais Jakaya Kikwete kwa taarifa yake ya mwisho wa mwezi na kusema ilikuwa na lengo la kuleta utulivu na amani japo kulikuwa na lawama kutoka kwa baadhi ya Wakristo na Waislamu.
‘’Kwa kweli ilikuwa na manufaa sana kwa Taifa tofauti na wengine walivyoichukulia, Rais hakupendelea upande wowote, ila lengo lake ni kuona watu wake wanaishi kwa amani’’.
Pia alimuomba Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Shaban Bin Simba kuharakisha uteuzi wa jopo la wawakilishi kwa ajili ya kukutana na Wakristo ili kujadili na kutafuta suluhu ya hali iliyopo nchini kwa sasa.
Kwa siku za karibuni kumekuwa na migogoro mbalimbali nchini ya kidini kati ya Wakristo na Waislamu huku kila upande ukisema sababu zake na kusababisha amani kwa baadhi ya maeneo kuyumba.
Wakuu wa mikoa Bungeni
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:27
- Hits: 102

Wakuu wa mikoa wakisoma hotuba ya bajeti ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2013/14 ilipokuwa ikiwasilishwa bungeni juzi. Picha na Edwin Mjwahuzi
Biashara barabarani
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:25
- Hits: 76

Wanyabiashara ndogondogo wakiwa wamepanga bidhaa zao katikati ya barabara ya Morogoro eneo la Manzese jijini Dar es Salaam kitu ambacho kimekuwa kikilalamikiwa na wakandrasi wa barabara hiyo kutokana na uharibifu wa baadhi ya miundombinu hiyo. Picha na Fidelis Felix
Hizi nayo!
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:21
- Hits: 91

Wananchi wakiangalia gari iliyotumbukia katika mtaro kando ya barabara ya Mandela karibu na ofisi za Mwananchi Communications Ltd (MCL) Dar es Salaam jana. Picha na Salhim Shao
Usafiri ziwani
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:19
- Hits: 78

Wakazi wa Mwamboa wa Ziwa nyasa Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe wakivuka katika ziwa hilo kwa kutumnia usafiri wa Mtumbwi. Picha na Said Ng'amilo.
Tuyapende mazingira yetu
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:17
- Hits: 89

Mkazi wa Kijiji cha Ndembo, Halmashauri ya Busokelo, wilayani Rungwe, Mbeya, akifanya usafi wa mazingira katika Soko la kijijini chao.
Usafi wa mazingira ni kitu cha lazima ili kuyaweka safi na kuepuka na hatari ya kupata magonjwa mbalimbali. Picha na Godfrey Kahango
''Tupendane jamani''
- Details
- Created on Friday, 12 April 2013 10:14
- Hits: 64

Katika jamii tunatofautiana kwa vitu vingi ikiwa ni pamoja na utofauti wa kipato, akili, uwezo wa kufanya kazi na kadharika. Inawezekana ni mpango wa Mungu ili tuweze kutumikiana kwa yeye mwenyewe anasema, ''huwezi kumpenda Mungu usiyemuona na kumchukia binadamu unayemuona
Tunahimizwa kupendana na kusaidiana kwa hali na mali na zaidi kwa wale wanaoonekana wanahitaji huruma hiyo zaidi.
''Hongera Uhuru''
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 09:06
- Hits: 80

Rais Jakaya Kikwete akimpongeza Uhuru Kenyatta kabla ya kuapisha jijini jana kuwa rais wa nne wa nchi hiyo. Katikati ni Naibu Rais wake, William Ruto. Picha na Mpiga Picha wetu. Nairobi
''Nitailinda nchi''
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 09:03
- Hits: 76

Rais wa awamu ya nne wa Kenyas Uhuru Kenyatta akionyesha upanga aliopokea kama nembo ya Taifa hilo kutoka kwa Rais anayemaliza muda wake Mwai Kibaki (kushoto) kwenye sherehe za kuapishwa kwake katika viwanja vya Moi International Sports Center Kasarani, Nairobi jana. Uhuru Kenyatta. Picha na AFP
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja, akijaribu moja ya magari aliyoyazindua
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 08:56
- Hits: 103

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja, akijaribu moja ya magari aliyoyazindua kuashiria uzinduzi wa kuwasafirishia Mahabusu kwenda Mahakamani kwa Mkoa wa Dodoma. Uzinduzi huo ulifanyika katika Gereza Kuu Isanga Dodoma jana. Picha na Felix Mwagara
Mchakato wa Katiba mpya kwenye asasi ya AFL
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 08:53
- Hits: 65

Mkazi wa Ilomba Ilomba Jijini Mbeya, Ruth Green, akisoma baadhi ya vifungu vilivyomo ndani ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mara baada ya asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Aman The Foudation Of Life (AFL) Kuwagawia katiba hizo walipofika katika kanisa na Baptist jana. Picha na Godfrey Kahango
Ukuta wa RTD wabomolewa
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 08:49
- Hits: 81

Wapita njia wakishangaa ukuta wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) uliovunjwa na Wakala wa barabara Tanroad katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam jana na kufanya kazi ya ulinzi wa eneo hilo nyeti, kuwa ngumu. Picha na Venance Nestory
Utendaji kazi waWizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo.
- Details
- Created on Wednesday, 10 April 2013 08:46
- Hits: 84

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,katika utekelezaji wa kazi za Wizara hiyo, Ikulu Mjini Zanzibar jana kwa ajili ya kuhakikisha huduma zitolewazo na wizara hiyo zinawasaidia ipasavyo wananchi. Picha na Mpiga Picha wetu
Msaada kwa wagunduzi na wajasiliamali nchini
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:56
- Hits: 116

Rafael Lubava, Mcl blog
Tume ya Sayansi na Teknolojia imetoa mfano hundi kwa wagunduzi na wajasiliamali sita wa Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA) zenye dhamani ya Tsh 82 milioni kwa wajasiliamali ili kuwasaidia kuendeleza shughuli zao walizoanzisha
Hundi hizo zilikabidhiwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa makao makuu ya COSTECH jijini Dar es Salaam jana baada ya kushinda mchakato uliokuwa na zaidi ya wajasiliamali 30 waliotuma maombi yao.
Profesa Mbarawa alisema msaada huo umetolewa ili kuwapunguzia changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kutokuwa na mitaji mikubwa, kutokuwa na vigezo vya kutosha kuomba mikopo na vitendea kazi vya kisasa.
‘’Changamoto zenu ni nyingi na Serikali kwa kutambua hilo, imetoa pesa hizo ili kuwasaidia kuendeleza ujasiliamali na ugunduzi wenu na hatimaye muweze kuwasaidia Watanzania wenzenu pia mvuke mipaka kama wengine’’. Alisema hayo na kuongeza.
Serikali imetenga Tsh bilioni 1.2 kwa ya kusaidia mfuko wa wabunifu wa sayansi na mawasiliano, mchakato mwingine utafanyika ili na wengine waweze kupata msaada utaowawezesha kufikia malengo yao’’.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi, Mhandisi George Mulamula amesema wajasiliamali na wabunifu wa hapa nchini ni lazima wawezeshwe kwa ajili ya manufaa ya Taifa na kuongeza ushindani wa Kimataifa.
‘’Wengi wao uwezo wao kifedha ni mdogo lakini wa uwezo kigunduzi wa vitu mbalimbali, ndio maana tumeanzisha mfuko utakaowasaidia katika tafiti zao ili kuhakikisha uwezo wao unatumika vizuri na kuleta manufaa kwa nchi nzima.
Wajasiliamali hao wameishukuru COSTECH na Serikali kwa msaada huo na kuahidi utatumika kama ilivyo pangwa kwa kuwa mtaji hawakuwa na fedha za kutekeleza shughuli zao.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa hundi hiyo, Dickson Ng’ang’a amesema inawezekana hata wao kuwa wajasiliamali wakubwa kama watapewa ushirikiano wa kutosha na kushauri ni vizuri kuwa waaminifu kwa msaada wanaopewa kuutumia kama ilivyokusudiwa.
Mfuko huo wenye lengo la kuwakwamua wajasiliamali nchini ili kuwasaidia kupata mahitaji mbalimbli ya kifedha na elimu, mbali na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia, mfuko huo unafadhiliwa pia na Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland.

Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akikabidhi mfano wa hundi kwa mjasiliamali na mgunduzi Mustapha Suleiman yenye thamani ya Tsh16 milioni kwa ajili ya kumsaidia katika shughuli zake. Picha na Rafael Lubava
Mtafutaji hachoki
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:41
- Hits: 73

Mwanamke wa jamii ya wafugaji akisuka mapambo ya shanga kwa ajili ya kuwauzia mbalimbali. Mama huyo pia huuza dawa za kienyeji katika eneo la Magomeni Kanisani jijini Dar es Salaam jana.Picha na Silvan Kiwale
''Hii ni kwa ajili ya masomo jamani''
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:38
- Hits: 76

Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo akizindua tovuti iitwayo www.shuledirect.co.tz jijini Dar es Salaam jana itakayosaidia wanafunzi wa sekondari kujifunza na kubadilishana ujuzi na wenzao kwa kutembelea tovuti hiyo. Wanaoshuhudia ni wanafunzi wa shule ya sekondari Kisutu.Picha na Silvan Kiwale
''Utajieleza kituoni''
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:36
- Hits: 85

Askari Polisi wa Kituo cha Polisi Buguruni akimwadhibu kijana ambaye haikujulikana kosa lake mbele ya Ofisi ya Upelelezi Mdogo na Dawati la Jinsia na Watoto baada ya kufikishwa katika kituo hicho jijini Dar es Salaam jana.Picha na Fidelis Felix
''Tulia''
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:35
- Hits: 63

Askari Kanzu wakimlinda kibaka aliyepewa kipigo na wananchi jana katika eneo la Buguruni Ghana baada ya kutenda uhalifu. Vibaka wamekuwa wakihatarisha maisha ya watu na mali zao kitu ambacho huleta kero sana. Picha na Venance Nestory
Ghai ''Nazindua''
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:32
- Hits: 65

Mwandamizi wa Katiba Institute ya Kenya, Yash Ghai akikata utepe mbele ya wajumbe wa kamati maalum ya katiba inayoratibiwa na kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwenye uzinduzi wake uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kamati hiyo itakuwa na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa watu kuhusiana na nchakato huo. Picha na Rafael Lubava
Kamati maalum ya katiba inayoratibiwa na kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
- Details
- Created on Tuesday, 09 April 2013 08:29
- Hits: 60

Mwenyekiti wa kikao cha kamati maalum ya katiba inayoratibiwa na kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Jenerali Ulimwengu akifafanua jambo wakati wa mkutano wa uzinduzi wake uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Picha na Rafael Lubava
Bilal atembelea Tume ya Sayansi
- Details
- Created on Thursday, 28 March 2013 09:23
- Hits: 128
Nora Damian,MCL
Dar es Salaam.Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal ameitaka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) kutumia wataalamu wa ndani kwa ajili ya kufanya tafiti zitakazosaidia nchi kuwa ya kisasa hasa katika fani za viwanda, tiba na kilimo.
Akizungumza jana baada ya kutembelea tume hiyo, Dk Bilal alisema serikali itaendeea kuongeza juhudi ili kuzalisha wataaamu wengi wa sayansi na teknolojia kwa ajili ya kuleta maendeleo.
Aliipongeza tume hiyo kwa kutoa ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi 219 kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza idadi ya wataalamu na kuwa na soko la ajira lenye tija.
“Tunatambua mchango mkubwa unaofanywa na Costech ili kuhakikisha nchi inapata wataalamu wengi wanaohusika na mambo ya sayansi na teknolojia,”alisema Dk Bilal.
Alisema kuna fursa nyingi ambazo hazikuwepo miaka ya nyuma lakini hivi sasa zinawea kutumiwa kutatua matatizo yaliyoko na kujiendeleza kiuchumi.
Awali Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Kuendeleza Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kilicho chini ya tume hiyo (DTBi) George Mulamula, alisema tangu kuanza kwa kituo hicho wamefanikiwa kujenga uwezo wa ndani na kutatua matatizo ya Watanzania katika teknolojia hiyo na kupunguza mzigo wa kibiashara kwa kampuni change.
Hata hivyo alisema wanakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwemo ukosefu wa mitaji ya kutosha kwa wajasiriamali, garama kubwa za vifaa vya mawasiliano na fikra potofu za baadhi ya vijana kutaka kuajiriwa badala ya kujiajiri wenyewe.

Dk. Bilal akiangalia moja ya vitabu vya wadau

Dk. Bilai akipata ufafanuzi wa jambo,katikati ni Mkurugenzi wa COSTECH, Hassan Mshinda

Mkurugenzi wa Vera Lab,(mwenye nguo nyekundu) akimweleza Makamu wa Rais, Dk. Gharib Bilal jinsi wanavyotoa huduma kwa shule zisizo na maabala kupitia huduma hiyo ilyopo kwenye gari.

Wadau wakifuatilia mtutano. Picha zote na Rafael Lubava
Mafundi TTCL
- Details
- Created on Thursday, 28 March 2013 09:10
- Hits: 94

Mafundi wa kampuni ya simu ya TTCL wakiunganisha nyaya zilizokatwa kwa bahati mbaya na wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi ya Strabag wakati wakichimba mtaro wa maji machafu katika eneo la Ubungo jijni Dar es Salaa.
Mkutano COSTECH
- Details
- Created on Thursday, 28 March 2013 09:06
- Hits: 85
Nora Damian,MCL
Dar es Salaam.Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) imepata msaada wa zaidi ya Sh 400 milioni kutoka kampuni ya Technobrain ambayo inajihusisha na masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano kwa ajili ya kukuza ujasiriamali na ubunifu.
Fedha hizo zimetolewa kupitia kituo cha kuendeleza teknolojia ya habari na mawasiliano (DTBi) ambacho kiko chini ya tume hiyo.
Akizungumza jana wakati wa kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dk Hassani Mshinda, alisema fedha hizo Dola 30,000 za Marekani zitasaidia wajasiriamali ambao wana makampuni yao ili yaweze kukua zaidi na kufanya kazi kwa ubora.
“Kuna vijana wengi ambao hawana mitaji wala ujuzi katika masuala mbalimbali hasa yanayohusu Tehama hivyo fedha hizi zitasaidia kupanua shughuli za DTBi ili ziweze kuwafikia watu wengi zaidi,”alisema Dk Mshinda.
Awali Ofisa Mtendaji Mkuu wa (DTBi) George Mulamula, alisema tangu kuanzishwa kwa kituo hicho hadi sasa wamefanikiwa kutengeneza ajira 4,500.
Pia alisema wameanzisha mfuko wa fedha wa kusaidia wajasiriamali na kwamba hadi sasa wameshapata Euro 100,000.
Alisema kupitia program mbalimbali zinazoendeshwa katika kituo hicho wameweza kusaidia vijana kuandika program ndogondogo kwenye simu kuhusu masuala ya afya, kilimo na biashara ambazo zimeonyesha mafanikio makubwa kwa sababu simu za mkononi zinatumiwa na watu wengi.

Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Hassan Mshinda akiongea kwenye mkutano.
Wajumbe wakiteta jambo wakati wa mapumziko mafupi

Wajumbe wa mkutano wakifuatilia mambo mbalimbali kwenye mkutano.
Haya ndio maisha yetu
- Details
- Created on Thursday, 28 March 2013 08:57
- Hits: 91
Maisha yana tofauti sana kutoka familia moja hadi nyingine, wakati wengine wakiwa hawana uhakika wa kula ,wengine wanakula na kusaza wao na mifugo yao, tena kuna familia nyingine husikia tu masuala ya kwenda katika hoteli kubwa kubwa.
Hali hiyo haikwepeki katika nchi yoyote duniani,lakini ni vizuri kuwa na huruma ya kujali wengine wasio nacho ili nao wajione wana haki ya kuishi.
Picha hizi zinaonyesha tofauti ya maisha kati ya watoto wa wenye uwezo na wasio nao.

watoto wakicheza kwenye chombo maalum cha michezo
Watoto wa mitaani wakiomba msaada abiria walioko kwenye daladala. Picha zote na Rafael Lubava
More Articles...
Wanaoperuzi SASA!
We have 12 guests and no members online
Banner One
Popular Blogs
- Daily Nation link (526 Hits)





